KAGUA
794
Tarehe ya kuingizwa:2012/04/10
Summary Maswali
katika nuio la ndoa ya muda mfupi, iwapo mwanamme atakuwa ni naibu na wakili wa mwanamke naye akalisoma nuio la ndoa baina yake na huyo mwanamke bila ya kutaja na kuainisha kiwango cha mahari na muda wa ndoa hiyo, je katika hali hiyo ndoa hiyo itakuwa imesihi?
SWALI
mimi nimeingia katika ndoa ya muda mfupi na mwanamme fulani, na mimi nilimuwakilisha yeye awe ni naibu wangu katika kuinuia ndoa hiyo, naye akaisoma na kuinuia ndoa hiyo bila ya kuainisha muda maalumu wala kiwango cha mahari ya ndoa hiyo. Je ndoa hii ni sahihi?
MUKHTASARI WA JAWABU

Jawabu kutoka kwa baadhi ya wanazuoni wetu ni kama ifuatavyo:

Ofisi ya kielimu ya Ayatu-Llahi Khamenei (Mungu amhifadhi) yenye kuhusika na kujibu maswali ya kifiqi, imetoa jawabu ifuatayo:

Iwapo mwanamke alimuakilisha mwanamme huyo kuisoma na kuinuia ndoa, pamoja na kumpa yeye uwakili wa kuainisha mahari pamoja na muda wa ndoa hiyo, ndoa hiyo haitakuwa na matatizo, lakini tu kinachotakiwa kuzingatiwa ni kwamba: ni wajibu kuchukua tahadhari katika kuifunga ndoa hiyo, yaani kunatakiwa zizingatiwe sharti za ndoa, na miongoni mwa sharti hizo, ni kutaka ruhusa kutoka kwa walii wa mwanamke, iwapo mwanamke huyo atakuwa ni bikra.

Ofisi ya kielimu ya Ayatu-Llahi Sistani (Mungu amhifadhi) yenye kuhusika na kujibu maswali ya kifiqi, imetoa jawabu ifuatayo:

Ndoa hiyo haina matatizo na imesihi.

Ofisi ya kielimu ya Ayatu-Llahi Makaarim Shirazi (Mungu amhifadhi) yenye kuhusika na kujibu maswali ya kifiqi, imetoa jawabu ifuatayo:

Iwapo mwanamme huyo alipewa unaibu wa kuifunga ndoa pamoja na unaibu wa kuainisha muda na mahari, basi ndoa yao itakuwa imesihi na haina mashaka.

Ofisi ya kielimu ya Ayatu-Llahi Safi Gulpegani (Mungu amhifadhi) yenye kuhusika na kujibu maswali ya kifiqi, imetoa jawabu hii:

Iwapo mwanamme atakuwa ameifunga ndoa hiyo kwa nia ya muda maalumu na mahari maalumu, lakini mwanamke akawa hana habari juu ya hilo, kisha mwamke huyo akapata habari baada ya muda fulani kuhusu kiwango cha mahari pamoja na muda halisi wa ndoa hiyo, ndoa yao itasihi.

Ofisi ya kielimu ya Ayatu-Llahi Mahdi Hadawiy Tehraniy (Mungu amhifadhi) yenye kuhusika na kujibu maswali ya kifiqi, imetoa jawabu ifuatayo:

Iwapo wewe (mwanamke) ulimpa huyo mwanamme uwakili wa yote hayo, yaani kuifunga ndoa pamoja na kuainisha muda na mahari, yaani wewe ulimpa mwanamme ruhusa ya kuanisha yeye mwenyewe muda anautaka na mahari anayo yataka. Ndoa yenu itakuwa ni sahihi, lakini iwapo wewe utakuwa hukumpa yeye aina hiyo ya uwakili na unaibu, basi usahihi wa ndoa hiyo utategemea ridhaa yako wewe baada ya wewe kujua na kufahamu kiwango cha mahari na muda wa ndoa alichokianisha mwanamme huyo, kwa hiyo kuridhika na kukubali kwako wewe juu ya hilo, ndiko kutakoifanya ndoa hiyo ipasi na iwe salama.

 

JAWABU KWA UFAFANUZI

Kwa ajili ya kunufaika zaidi kuhusiana na masuala ya ndoa ya muda mfupi, angalia maswali yafuatayo katika tuvuti yetu:

1- Swali namba 1238: kuhusiana na masharti ya ndoa za muda mfupi, namba ya swali kwenye tovuti ni 1225.

2- Swali namba 2190: kuhusiana na ndoa ya muda mfupi kwa aliyekuwa bikra, namba ya swali katika tovuti ni 2315.

2- Swali namba 3237: kuhusiana na ulipaji wa mahari ya ndoa ya muda mfupi, namba ya swali katika tovuti ni 3494.

4- Swali namba 7454: kuhusiana na kuyaelewa mashati ya ndoa ya muda mfupi, namba ya swali katika tovuti ni 7664.

TARJAMA YA JAWABU KATIKA LUGHA NYENGINE
MAONI
Tafadhali ingiza thamani
mfano : Yourname@YourDomane.ext
Tafadhali ingiza thamani
Tafadhali ingiza thamani

MASWALI KIHOLELA

YALIYOSOMWA ZAIDI

  • je ni kweli kuwa Maimamu ni wabora zaidi kuliko hata Mitume?
    1240 Elimu ya zamani ya Akida 2012/05/23
    Suala la Maimamu (a.s) kuwazidi Mitume katika daraja za kielimu, ni suala moja linalo onekana kuzungumziwa sana na Riwaya mbali mbali, na sababu hasa za wao kuwazidi Mitume kielimu, zinatokana na ule uhakika wa nuru ya maumbile yao, kwani uhakika wa nuru yao unatokana na uhakika wa nuru ya Mtume ...
  • kuna tofauti gani baina ya tabia na eimu ya tabia (saikolojia)?
    1227 Tabia kimtazamo 2012/06/17
    Neno (tabia) linatokana na neno la Kiarabu (اخلاق) ambalo ni umoja wa neno (خُلْق) lenye maana ya tabia, nyenendo au sifa za watu mbali mbali zinazo zimbatana na matendo yao bila ya kutofautisha baina ya sifa na tabia mbaya na zile sifa njema. Wataalamu wa elimu ya tabia (saikolojia) na wanafalsafa ...
  • kwa nini Imamu Husein (a.s) anaitwa Tharu-Llahi (ثار الله)?
    1208 Tabia kimtazamo 2012/05/23
    Neno Tharu-Llahi (ثار الله) limekuja likiwa na maana mbili: moja ni kwa maana ya damu, na ya pili ni kwa maana ya kulipiza kisasi na kutaka kummwga damu ya muuwaji. Kwa hiyo maana ya mwanzo inapotumika kwa ajili ya kumuita Yeye (a.s) Tharu-Llahi (ثار الله), huleta maana ya kuwa: Mola weke ...
  • nini maana ya neno (dini)? Au dini hasa ni kitu gani?
    1108 Falsafa ya Dini 2012/05/23
    Wamagharibi wametumia ibara mbali mbali ili kupata maana muwafaka inayowafikiana na neno (dini), na neno (dini) ndani ya Qur-ani limetumika huku likibeba maana mbili tofauti, nazo ni kama ifuatavyo: 1- dini ni aina yeyote ile ya itikadi yenye kulenga nguvu maalumu za ghaibu zinazoaminiwa na kundi fulani la waumini wa nguvu ...
  • nini maana ya itikafu
    1090 Tabia kimtazamo 2012/05/23
    Neno (itikafu) kilugha, huwa lina maana ya kule mtu kukaa na kubaki katika sehemu au pahala maalumu, huku akiwa ameshikamana na jambo maalumu ndani ya mahala hapo, lakini neno hili kitaalamu (kwenye fani ya sheria za Kiislam) linamaanisha kule mtu kukaa katika sehemu takatifu kwa ajili ya kutaka kujikaribisha kwa ...
  • kwa mtazamao wa Kiislamu, mwanaadamu ni kiumbe gani?
    1090 Elimu mpya ya Akida 2012/05/26
    Kwa mtazamo wa Qur-ani, mwanaadamu ni kiumbe aliyebeba sifa mbili tofauti za kimaumbile, moja ni ile inayotokana na maumbile aliyopewa tokea mwanzo kutoka kwa Mola wake, nayo ni maumbile ya kiroho, na ya pili inatokana na maumbile ya kiwiliwili alichonacho. Maumbile asili ya kiroho (kifitra), huwa ni yenye kiu ya ...
  • kwanza kabisa napenda kuuliza kuwa: je watu wa Peponi wote watakuwa ni vijana? Na la pili ni kwamba: imekuwaje miongoni mwa Maimamu wote pamoja na Mtume (s.a.w.w), ikawa Imamu Hasan na Husein tu ndio mabwana wa vijana wa Peponi?
    1082 Elimu ya zamani ya Akida 2012/05/23
    Wajukuu hawa wawili wa Mtume (s.a.w.w) ni mabwana wenye utukufu juu ya vijana wote Peponi, haidhuru kuwa ndani ya Pepo watu wote watakuwa katika hali moja ya ujana, ama wao (Imamu Hasan na Husein (a.s)) ndio watakaong’ara zaidi katika wale vijana waliouwawa katika njia ya Mola, au wale waliofariki katika ...
  • nini maana ya usemi usemao kuwa: kumzuru Imamu Husein (a.s) ni sawa na kumzuru Mola kwenye Arshi yake”?
    1062 Elimu ya zamani ya Akida 2012/05/23
    Imamu Husein bin Ali (a.s) ambaye ni Imamu wa tatu wa Kishia, ni mtu mwenye fadhila kubwa mbele ya Mola wake, na fadhila hizo amezipata kwa kutokana na malengo yake, matendo, kutojitanguliza mbele katika maslahi ya jamii yake pamoja na kule kujitoa keake muhanga kwa ajili ya dini na manufaa ...
  • nini maana ya ucha Mungu?
    1059 Tabia kimtazamo 2012/05/23
    Taqwa (ucha Mungu) ni nguvu maalumu za kiroho zinazo weza kupatikana ndani ya nafsi ya mwanaadamu, nguvu ambazo huwa ni himaya maalumu inayomuwezesha yeye kujitenga na maasi. Taqwa kamili ni ile inayomfanya mtu kujiepusha na maasi yanayo eleweka na kila mmoja wetu, pamoja na kujiepusha na yale yote yanayo dhaniwa ...
  • hivi ni kwa nini Imamu Ali (a.s), hakuamua kilinda nafsi yake mbele ya adui yake (Ibnu Muljim), hali ya kuwa Yeye (a.s) alikuwa akielewa vyema nia ya adui huyo?
    1023 Elimu ya zamani ya Akida 2012/05/23
    Jawabu kamili ya swali hili yaweza kukamilika kuvitambua vipengele vifuatavyo: Vigezo halisi kwa mja katika utendaji wa amali na nyadhifa zake zinazomfungamanisha na wanajamii mbali mbali, ni ile elimu yake ya kawaida. Imamu (a.s) huwa hatumii nguvu zake za ndani zinazotokana na utukufu wa roho yake ambazo ni zenye kushikamana na ulimwengu ...

MAFUNGAMANO