advanced Search
KAGUA
12932
Tarehe ya kuingizwa: 2010/11/08
Summary Maswali
je ndani ya mchana wa Ramadhan iwapo mtu yeye pamoja na mkewe atakuwa hakufunga, hivi ataruhusiwa kulala na mkewe ndani ya mchana huo?
SWALI
je iwapo atakuwa hakufunga kwa kutokana na moja kati ya dharura fulani, mtu huyo ataruhusiwa kulala na mkewe ambaye vile vle yuko nje ya funga? Au ni vibaya kufanya hivyo ndani ya Ramadhani?
MUKHTASARI WA JAWABU

Ndani ya fatwa za wanazuoni, kuna mambo 9 ya msingi yenye kubatilisha saumu, nayo ni: 1- kula na kunywa, 2- kujamii, 3- kupiga ponyeto, 4- kumzulia uongo Mola na Mtume wake pamoja na maimamu (s.a.w.w), 5- kuingiza vumbi zito kooni, 6- kuzamisha kichwa majini, 7- kubaki na janaba, hedhi au nifasi hadi wakati wa adhana ya asubuhi, 8- kutumia aina fulani ya ulevi na la 9- ni kutapika.[1] Mambo tisa yaliyotajwa hapo, yote ni yale mambo yenye kubatilisha saumu, na siyo mambo ambayo ni haramu kuyatenda ndani ya mwezi wa Ramadhani. Hivyo basi iwapo mke na mume watakuwa wako nje ya saumu, wanaweza kulala pamoja. Lakini Wanazuoni wa kifiqhi, wamesema kuwa: kufanya hivyo ni makruhu (aipendezewi) kwa yule asiyekuwa na saumu, na hukumu ya tendo hilo kwa wale wasiokuwa na saumu ni makruhu.[2]

 


[1] Taudhihul-Masaail kilicho shereheshwa na Imam Khomeiniy, juz/1, uk/891, suala la 1572, kilochapishwa na Muasasatu Nashru Islamiy, kitengo chenye fungamano na Jamiatul-Mudarrisiin, Qum, chapa ya nne ya mwaka 1424 Hijiria Qamaria.

[2] Taudhihul-Masaail kilicho shereheshwa na Imam Khomeiniy, juz/1, uk/955.

 

TARJAMA YA JAWABU KATIKA LUGHA NYENGINE
MAONI
Idadi ya maoni 0
Tafadhali ingiza thamani
mfano : Yourname@YourDomane.ext
Tafadhali ingiza thamani
<< Niburute.
Tafadhali ingiza kiasi sahihi ya usalama Kanuni

MPANGILIO WA KIMAUDHUI

MASWALI KIHOLELA

YALIYOSOMWA ZAIDI