advanced Search
KAGUA
14138
Tarehe ya kuingizwa: 2018/11/11
Summary Maswali
Vipi talaka hutimia, maneno gani hutumika kwa ajili ya talaka, na ni mara ngapi?
SWALI
Vipi talaka hutimia, maneno gani hutumika kwa ajili ya talaka, na ni mara ngapi?
MUKHTASARI WA JAWABU
Kulingana na madhehebu ya Shia, iwapo mtu atakasirika kupita budi, kiasi ya kwamba akawa ametoa talaka bila ya makusudia au bila ya hiari kwa kutokana na kutawaliwa na hasira kupita budi. Hapo talaka haitakutimia. Ila kama atakuwa amekasirika kupitia budi, ila bado yupo timamu na akawa ametoa talaka kwa makusudio kamili na kwa hiari yake, basi talaka itakuwa imetimia.
Jawabu ya swali lako utaipata kupitia namba maalimu inayohusiana na swali lako.
Baadi ya madhehebu ya Kiislamu, yamelilainisha mno suala la talaka limepewa njia nyepesi kupita budi katika ukubalikaji wake, jambo ambalo limesababisha katika zama zetu hizi suala la talaka kuonenaka ni kama mchezo tu. Ama kwa upande wa madhehemu ya Shia, suala hili linaangaliwa kupitia ngazi tofauti katika kupokelewa na kukubalika kwake. Kishia talaka ni hukumu yenye toleo la upande mmoja, yaani mume ndiye mwenye haki ya kutoa talaka. Wakati wowote ule mume anaweza kumuacha mkewe kupitia mfumo ufuatao:
    Talaka ni lazima isomwe kwa lugha ya Kiarabu kupitia ibara maalumu kma vile «زَوْجَتِى فٰاطِمَةُ طالِقٌ» yaani mke wangu Fatuma ameshaachika, na iwapo atamuwakilisha mtu kumwacha mkewe, basi wakili huyo atasema «زَوْجَةُ مُوکِّلى فٰاطِمَةُ طٰالِقٌ» yaani mke wa mwakilishwa wangu ambaye ni bibi Fatuma ameshaachika.
   Ili talaka itimie ni lazima zizingatiwe sharti zifuatazo:
1- Mwachaji (mume) ni lazima awe ni mwenye akili timamu, na mwachaji kuwa ni baleghe pia ni sisitizo la wajibu. Pia awe hakulazimishwa bali kaacha kwa hiari yake, na iwapo atakuwa amelazimishwa amwache mkewe, talaka hiyo haitosihi.
2- Mtoaji talaka awe amekusudia kutaliki, kwa hiyo kama ataisoma ibara ya talaka kimchezo (kiutani), talaka hiyo haitosihi.
3- Anayeachwa awe yupo tohara, yaani asiwe katika hali ya hedhi au nifsi, na mumewe awe hajamuingilia (hajatenda naye tendo la ndoa) ndani ya tohara hiyo. Yaani awe bado hajawahi kumuingilia baada ya kutoharika, la ikiwa amemuingilia, basi itambidi asubiri hadi aingie katika hedhi kwa mara nyengine kisha atoharike, baada ya kutoharika asije kumuingilia, hapo ndipo anaweza kumpa talaka.
Ila kuna sura tatu ambazo yawezekana mke kutalikika (kuachika) huku akiwa ndani ya hedhi au nifasi;
A- Mume baada ya kuoana na mke huyo awe hajawahi kutenda naye tendo la ndoa ambalo limetimia, yaani kukutana kwa tupu mbili ambapo sehemu ya matahiriyo ikawa imezama katika tupu ya mwanamke.
B- Iwapo mke atakua na mimba, katika ambayo mume atakuwa amemuacha mkewe huku akiwa na hedhi, katika hali ya kuto kujua kuwa ana mimba, kisha tena baadaye akafahamu kuwa yeye alipomuacha alikuwa katika hali ya ujauzito, basi talaka itakuwa imefaa.
C- Iwapo mume atakuwa yupo mbali na ikawa ni vigumu (hakuna uwezekano) yeye kufahamu kuwa mkewe yupo ndani ya hedhi au ameshatoharika. Hapo talaka itasihi.
4- Iwapo mume atamuoa mwanamke, kisha akamuacha kabla ya kutenda naye tendo la ndoa. Hapo mume atawajibika kumpa mwanamke huyo nusu ya mahari waliyokubaliana hapo mwanzo walipomuoana. Ama akiwa tayari ameshatenda naye tendo la ndoa, basi ni wajibu wa mume kumlipa mwanamke huyo mahari yake kalimi.
5- Iwapo tamko la talaka litatoka mara moja na shuruti zake zikawa zimekamilika, basi hakuna haja kurudia tena ibara hiyo kwa mara ya pili. Na kwa mara hiyo hiyo moja talaka itakuwa imeshatoka na kukamilika na mke atakuwa tayari ameshaachika. Iwapo mke na mume wataachana   mara mbili kisha wakarudiana, iwapo atamuacha tena mara ya tatu, hapo haitokubalika wao kurudiana. Na mke atakuwa ni haramu kudiwa tena na mume huyo. Ila kama mke huyo baada ya kumalizika eda ataolewa na mume mwengine kisha akaachwa, hapo mume wa mwanzo anaweza kumuowa tena mke huyo baaya kwishwa eda yake. Pia ni lazima huyo mume ambaye atamuowa baada ya lalaka hiyo ya tatu, ni lazima awe ni baleghe na mwenye aliki timamu, na vile vile ni lazima amuingilie na awe amemuoa kwa nia ya kuishi naye ndoa ya daima. Pia yawezekana ikaulizwa je hivi inajuzu katika kikao kimoja mume akatoa talaka moja kisha hapo hapo akamrudia mkewe hali mke akiwa hayupo kikaoni, kisha akamuacha tena papo hapo. Je talaka ya aina kama hii itajuzu? Wanazuoni wamekhtalifiana juu ya jambo hili. Wenge wansema yawezekana, na wengine amekataa. Waliosema yawezekana wamedai kuwa si lazima katika kumrudia mke kupite tendo la ndoa au mke awepo katika kurudiwa huko, ila kama sharti za talaka zitatimia basi talaka itakuwa imesihi.
6- Iwapo mke ataachika basi ni lazima asubiri hadi apitiwe na hedhi mbili na tohara mbili, na atakapoingia katika hedhi ya tatu, hapo eda itakuwa imemalizika, na aweza kuolewa tena. Na iwapo mwanamke atakuwa haingii katika hedhi lakini umri wake ni wa kuingia hedhi, kisha akaachwa, basi katika hali hiyo ya yeye kutoona hedhi (pengone ni mgonjwa), eda yake itakuwa ni miezi mitatu. Eda ya ya mtu mwenye mimba ni hadi kujifungua, akijifungua tu eda itakuwa imemalizika. Au iwapo ataharibu, yaani mimba yake ikaharibika na mtoto akatoka kambla ya muda, pia yeye eda yake itakuwa ni baada ya kuharibika kwa mimba hiyo.
Ama kuhusiana na ndoa ya muda (mut’a) ambayo ni yenye kukubalika katika madhehebu ya shia, talaka ya ndoa hii baada ya kumalizika muda waliyokubaliana, au mume kusamehe muda uliobakia. Na eda yake ni hedhi mbili, yaani baada ya mwanamke kuungia katika hedhi mara mbili na kutohariaka. Na kwa wale wasioona hedhi eda yao ni siku 45.
 
Kwa hiyo kuhusiana na kupita talaka kwa sms, hapo yatupasa kuangalia hali na sharti za talaka tulizokufafanulia katika makala hii. Lakini kwa kukusaidia tu ni kwamba; iwapo yeye atamuakilisha mtu amtaliki mkewe, kisha pia wakawepo mashahidi adilifu katika kuishuhudia talaka hiyo. Hapo bila shaka talaka itasihi, na wala hapatakuwa na pingamizi juu yahilo.
 
 
TARJAMA YA JAWABU KATIKA LUGHA NYENGINE
MAONI
Idadi ya maoni 0
Tafadhali ingiza thamani
mfano : Yourname@YourDomane.ext
Tafadhali ingiza thamani
<< Niburute.
Tafadhali ingiza kiasi sahihi ya usalama Kanuni

MPANGILIO WA KIMAUDHUI

MASWALI KIHOLELA

  • Vipi mtu anaweza kuwa kipenzi cha Mwenye Ezi Mungu?
    8835 Tabia kimatendo 2019/06/16
    Katika lugha ya Kiarabu, -ambayo ndiyo lugha ya sheria ya Kiislamu- neno (pendo) linatokana na neno "حب". Ambalo lina maana ya kule mtu kuwa na mapenzi na mtu, kitu au jambo fulani. Lakini neno pendo, mapenzi au neno jengine lenye maana kama hii, linapotumika na kunasibishwa ...
  • je mtu asiwajibikiwa kufunga (asiyefunga) ana ulazima wa kutoa zakatul-fitri?
    11954 زکات فطره 2012/05/23
    Mtu atakaeingiliwa na usiku wa Idil-fitri, huku akiwa ni baleghe na mwenye akili timamu, naye akiwa si mtumwa wa mtu wala si fakiri, mtu huyo atawajibika kutoa zakatul-fitri kwa ajili yake na kwa ajili ya wale wote anaowahudumia, na kiwango cha kila mmoja ni kiasi cha kilo ...
  • maadili mema yana nafasi gani kwenye uwanja wa mazoezi?
    12966 Tabia kimatendo 2012/05/23
    Uisalmu ni dini kamili iliyokusanya ndani yake mfumo kamili na salama wenye kutoa muelekeo wa kiutendaji kuhusiana na kipengele kimoja kimoja miongoni mwa vile vipengele vinavyo husiana na maisha ya mwanaadamu. Uislamu haukuliweka nyuma suala la afya ya mwili wa kila mmoja wetu. Kwa hiyo Uislamu ni ...
  • kwa nini Uislamu unaamuru kuwanyonga wanaoritadi? Je hilo haliendani kinyume na uhuru wa kila mmoja kuabudu anacho kitaka?
    22870 حدود، قصاص و دیات 2012/05/23
    Kuritadi ni kitendo cha wazi kabisa cha kutoka katika dini, na mara nyigi tendo hilo hutumika kama ni nyenzo ya kuwadhoofisha wengine kiimani na kuwafanya waache dini yao, na hatimae kuwatoa na kuwaweka nje ya dini. Wanaohukumiwa hukumu ya kuritadi, ni wale wanaolidhihirisha tendo hilo kwa wengine, ...
  • nini maana ya itikafu
    21325 اعتکاف 2012/05/23
    Neno (itikafu) kilugha, huwa lina maana ya kule mtu kukaa na kubaki katika sehemu au pahala maalumu, huku akiwa ameshikamana na jambo maalumu ndani ya mahala hapo, lakini neno hili kitaalamu (kwenye fani ya sheria za Kiislam) linamaanisha kule mtu kukaa katika sehemu takatifu kwa ajili ya ...
  • je kitabu cha tarehe kijulikanacho kwa jina la Taarekhu-Tabari, ni kitabu kinachoaminika?
    10553 امام حسین قبل از امامت 2012/05/23
    Pale kitabu fulani kinaposemekana kuwa ni chenye kuaminika, huwa haimaanishi kuwa kila kilichomo ndani yake ni sahihi. Kitabu Taarikhut-Tabariy, si chenye kuepukana na usemi huu, bali nacho pia hakikubeba ndani yake yale yalio sahihi tu. La pili ni kwamba: kauli hiyo ulioinukuu kutoka katika kitabu hicho ...
  • je ni kweli kuwa Maimamu ni wabora zaidi kuliko hata Mitume?
    16934 دانش، مقام و توانایی های معصومان 2012/05/23
    Suala la Maimamu (a.s) kuwazidi Mitume katika daraja za kielimu, ni suala moja linalo onekana kuzungumziwa sana na Riwaya mbali mbali, na sababu hasa za wao kuwazidi Mitume kielimu, zinatokana na ule uhakika wa nuru ya maumbile yao, kwani uhakika wa nuru yao unatokana na uhakika wa ...
  • nini hukumu ya kufuga njiwa ndani ya sheria za Kiislamu? Na nini msingi hasa wa hukumu hiyo?
    26426 نگهداری و شکار حیوانات 2012/06/17
    Tukilitazama suala la kufunga njiwa kibinafsi, tutalikutia kuwa suala hili halina matatizo na ni halali. Lakini pale sisi tutapolimbatanisha suala hili na haki za majirani au wanajamii, hapo tunaweza kulipa picha ya uhalali au uharamu kwa jinsi hali za jamii mbali mbali zinavyolitazama suala hilo. Baadhi ya ...
  • Je ni kweli kuwa Imamu Husein (a.s) aliwahi kuwa na binti mwenye umri wa miaka mitatu au mine, aliyejulikana kwa jina la Ruqayya au Sukaina anaye semekana kuwa alifariki dunia huko Damascus?
    11645 اهل بیت و یاران 2012/05/23
    Ingawaje wengi miongoni mwa waandishi wa Historia hawakukinukuu kisa cha kuwepo kwa mtoto huyo wa kike wa Imamu Husein (a.s) mwenye umri wa kiasi cha miaka mitatu au mine, aliyejulikana kwa jina la Ruqayya au Fatimatu Sughra na baadhi ya wakati akijulikana kwa majina yasiokuwa hayo, lakini ...
  • je dini na siasa ni vyenye kuendana au vyapingana?
    14099 Elimu mpya ya Akida 2012/05/23
    Dini ni chombo maalumu kilichokuja kumkomboa mwanaadamu na kumuongoza katika njia ya mafanikio, hivyo basi ni jambo lisiloingia akilini kuwa chombo hichi kiwe ni chenye kulipa mgongo jambo muhimu linalohitajika ndani ya jamii mbali mbali, kama vile suala la usimamishaji wa serikali. Na kwa upande mwengine ni ...

YALIYOSOMWA ZAIDI