advanced Search
KAGUA
15772
Tarehe ya kuingizwa: 2010/06/27
Summary Maswali
ni zipi funga zilizo zisizofaa kwa mtazamo wa imam Shafi, Hanafi na Maalik?
SWALI
ni zipi funga zilizo zisizofaa kwa mtazamo wa imam Shafi, Hanafi na Maalik?
MUKHTASARI WA JAWABU

Masiku yasiyofaa kufunga saumu mbele ya imam Abu Hanifa ni: siku ya idi ndogo na idi kubwa, pia kufunga siku ya mwezi 11, 12 na 13 ya mwezi wa Dhil-hijja, pia kufunga ndani ya idi pili hadi nne za idi ya mfunguo tatu.

Funga zisizofaa kwa mtazamo wa imam Shafi ni: kufunga siku ijulikanayo kwa jina la yaumu shaka, kufunga siku ya idi ndogo na kubwa, vile vile kufunga ndani ya idi pili hadi nne za idi ya mfunguo tatu, iwe mtu yupo kwenye ibada ya hija au nyumbani, kufunga kabla ya kuingia mwezi wa Ramadhani kwa siku moja au mbili pia ni haramu, kufunga kwa kuanzia nusu ya pili ya Shaabani iwapo utakuwa hukuanza kufunga tanga mwanzo wa mwezi huo, ila tu unaruhusiwa kufunga ndani ya masiku hayo pale utapokuwa umeweka nadhiri ya funga au kwa mwanamke ambaye ana dharura ya kuzilipa funga zake zilizompita kwa kutokana na dharura za uke (hedhi).

JAWABU KWA UFAFANUZI

A - funga zisizofaa mbele ya imam Abu Hanifa ni kama ifuatavyo:

1- haifai kufunga katika siku ya kuchinja katika ibada ya hija: na iwapo mtu ataweka nadhiri ya kufunga katika siku hiyo, nadhiri yake haitohesabiwa kuwa ni nadhiri inayokubalika, kwa kule kuharamika kwa saumu ndani ya siku kama hiyo, na ni maasi kufunga ndani ya siku hiyo.[1]

2- kufunga siku ya idi ndogo na idi kubwa pamoja na siku tatu baada ya Idul-adh-haa ambayo ni idi inayofanyika baada ya ibada ya hija haifai kufunga ndani yake, na kufunga ndani ya siku tatu hizo ni Makruhu iliyo kubwa kabisa (مکروه تحریمی)  isipokuwa kwa yule atakayekuwepo ndani ya ibada ya hija.[2]

3- ni Makruhu kufunga ndani ya masiku ya Ayyaami tashriiq, nayo ni mwezi 11,12 na 13 ya Dhil-hijja.[3]

Mahanafi (watu wa madhehebu ya Hanafiy), hulitumia neno (مکروه تحریمی), wakimaanisha tendo lililo karibu na uharamu.[4]

B- funga zisizofaa mbele ya imam Shafi ni:

1- kufunga ndani ya siku ya Yaumu shaka ni Haramu hadi mwezi uonekanae.[5]

2- ni Haramu kufunga siku ya Idul-Fitr na Idul-Adh-haa, ambazo ni zenye kujulikana kwa jina la siku kuu ndogo na siku kuu kubwa, pia ni Haramu kufunga siku tatu baada ya Idul-Adh-haa, wala hakuna tofauti baina ya yule aliyekuwemo ndani ya ibada ya hija au yule asiye kuwepo kwenye ibada hiyo.[6]

3- ni Haramu kufunga siku moja au mbili kabla ya kuingia mwezi wa Ramadhan.[7]

4- ni haramu kufunga kwa kuazia nusu ya pili ya Shaabani iwapo mtu atakuwa hakuanza kufunga tokea mwanzoni mwa Shaabani, kwa hiyo hakutokuwa na tatizo kwa yule aliye anza kuufunga mwezi huo tokea mwanzoni mwake na kuuendeleza hadi uwezo wake utavyomruhusu.[8]

5- ni haramu kufunga saumu kwa mtu ambaye saumu kwake ni yenye kumletea madhara, kiasi ya kwaba iwapo atafunga basi aweza kupoteza kimoja kati ya viungo vya mwili wake, au itakapo khofiwa kuhiliki mtu huyo kwa kutokana na kufunga.[9]

6- ni haramu mke kufunga saumu ya Sunna bila ya idhini ya mumewe, iwapo funga hiyo itasababisha kupotea kwa haki za mume huyo, hiyo ni kwa sababu mke anatakiwa kufuata amri za mumewe.[10]

C- funga zisizofaa kwa mujibu wa mtazamo wa imam Maalik:

1- ni haramu kufunga kabla ya kuonekana kwa mwezi wa Ramadhani hadi mwezi uandame, hata kama mwezi wa Shaabani utakuwa umeshazidi zaida ya siku thalathini.[11]

2- ni Haramu kwa mwanamke kufunga funga ya Sunna bila ya idhini ya mumewe, iwapo funga hiyo itasababisha kupotea kwa haki za mume huyo, hiyo ni kwa sababu mke anatakiwa kufuata amri za mumewe.[12]

3- ni Haramu kufunga ndani ya siku ya idi ya baada ya Ramadhani na idi ya Mfunguo tatu.[13]

4- ni Haramu kufunga mwezi11, 12 na 13 za mwezi wa Dhul-Hijja, ambazo ni baada ya idi tu.[14]

5- ni Haramu kufunga siku ya shaka (yaumu shaka), yaani siku ambayo inatiliwa shaka na haieleweki kuwa ni ya mwezi wa Shaabani au Ramadhani.[15]

 

 


[1] Kitabu Tabyinul-Haqaaiq wa haashiatu Al-Shabliy, mlango wa funga, kipengele kisemacho (فَصْلٌ نَذَرَ صَوْمَ يَوْمِ النَّحْرِ) cha Fakhrudi-diin  Al-Zai-iliy  Al-Hanafiy, Uthman bin Ali bin Muhjin Al-Baari-iy.

[2] Alfiqhu alaa madhaahibil-arba-a wa madhabu Ahli-bait, juz/1 uk/720, chapa ya kwanza ya Daruth- thaqalain ya mwaka 1419 Hijiria, pia Al-fiqhu alaa madhaahibul- khamsa cha Muhammad Jawad Al-Mughniya, juz/1 uk/160, chapa ya kwanza ya Daru tayyaril-jadiid-Darul- Jawad Beirut, mwaka 1421 Hijiria.

[3] Alfiqhu alaa madhaahibil-khamsa, juz/1, uk/161.

[4] Rejea kitabu kilichopita, uk/160.

[5] Majmu-u fatawa wa rasaail fadhilatu sheikh Muhammad bin Saleh  Al-Uthaimin, cha Muhamma bin Saleh bin Muhammad Al-Utahaimin, mlango wa funga, kipengele cha, funga ya kujikaribisha kwa Mola, ambacho ni kitabu kilichoandikwa kwa Kiarabu, na muongozo wake wa rejeo hii kwa Kiarabu ni kama ifuatavyo:

. کتاب الصیام، « صیام التطوع »، مسائل من کتاب الفروع، المسألة الاولی، القول الخامس.

[6] Fiqhi alaa mdahahibil-arba-a wa madhabi Ahlul-Bait, juz/1, uk/720, pia Fiqhu alaa mdahahibil-khamsa, juz/1, uk/160.

[7] Fiqhu alaa mdahahibil-arba-a wa madhabi Ahlul-Bait, juz/1, uk/726.

[8] Rejea ki kitabu kilichopita.

[9] Rejea kitabu hicho hicho, uk/727.

[10] Kitabu kilichopita, uk/720 hadi 721, pia uk/727. Pia kitabu Fiqhu alaa mdahahibil-khamsa, juz/1, uk/161.

[11] Majmu-u fatawa wa rasaail Fadhilatu sheikh Muhammad bin Saleh Al- Uthaimin, na bayana yake kwa kiarabu ni kama ifuatavyo:

مجموع فتاوى ورسائل فضيلة الشيخ محمد بن صالح العثيمين، کتاب الصیام، « صیام التطوع »، مسائل من کتاب الفروع، المسألة الاولی، القول الخامس.

[12] Alfiqhu alaa mdahahibil-arba-a wa madhabi Ahlul-Bait, juz/1, uk/720 hadi 721, pia uk/727, pia rejea kitabu Alfiqhu alaa madhahibil-khamsa, juz/1, uk/161.

[13]  Kitabu kilichopita, uk/720, pia  kutabu kilichopita, uk/160.

[14] Kitabu kilichopita, uk/160 hadi 161.

[15] Alfiqhu alaa mdahahibil-arba-a wa madhabi Ahlul-Bait, juz/1, uk/720.

 

TARJAMA YA JAWABU KATIKA LUGHA NYENGINE
MAONI
Idadi ya maoni 0
Tafadhali ingiza thamani
mfano : Yourname@YourDomane.ext
Tafadhali ingiza thamani
<< Niburute.
Tafadhali ingiza kiasi sahihi ya usalama Kanuni

MPANGILIO WA KIMAUDHUI

MASWALI KIHOLELA

  • Vipi mtu anaweza kuwa kipenzi cha Mwenye Ezi Mungu?
    8835 Tabia kimatendo 2019/06/16
    Katika lugha ya Kiarabu, -ambayo ndiyo lugha ya sheria ya Kiislamu- neno (pendo) linatokana na neno "حب". Ambalo lina maana ya kule mtu kuwa na mapenzi na mtu, kitu au jambo fulani. Lakini neno pendo, mapenzi au neno jengine lenye maana kama hii, linapotumika na kunasibishwa ...
  • je mtu asiwajibikiwa kufunga (asiyefunga) ana ulazima wa kutoa zakatul-fitri?
    11954 زکات فطره 2012/05/23
    Mtu atakaeingiliwa na usiku wa Idil-fitri, huku akiwa ni baleghe na mwenye akili timamu, naye akiwa si mtumwa wa mtu wala si fakiri, mtu huyo atawajibika kutoa zakatul-fitri kwa ajili yake na kwa ajili ya wale wote anaowahudumia, na kiwango cha kila mmoja ni kiasi cha kilo ...
  • maadili mema yana nafasi gani kwenye uwanja wa mazoezi?
    12966 Tabia kimatendo 2012/05/23
    Uisalmu ni dini kamili iliyokusanya ndani yake mfumo kamili na salama wenye kutoa muelekeo wa kiutendaji kuhusiana na kipengele kimoja kimoja miongoni mwa vile vipengele vinavyo husiana na maisha ya mwanaadamu. Uislamu haukuliweka nyuma suala la afya ya mwili wa kila mmoja wetu. Kwa hiyo Uislamu ni ...
  • kwa nini Uislamu unaamuru kuwanyonga wanaoritadi? Je hilo haliendani kinyume na uhuru wa kila mmoja kuabudu anacho kitaka?
    22870 حدود، قصاص و دیات 2012/05/23
    Kuritadi ni kitendo cha wazi kabisa cha kutoka katika dini, na mara nyigi tendo hilo hutumika kama ni nyenzo ya kuwadhoofisha wengine kiimani na kuwafanya waache dini yao, na hatimae kuwatoa na kuwaweka nje ya dini. Wanaohukumiwa hukumu ya kuritadi, ni wale wanaolidhihirisha tendo hilo kwa wengine, ...
  • nini maana ya itikafu
    21325 اعتکاف 2012/05/23
    Neno (itikafu) kilugha, huwa lina maana ya kule mtu kukaa na kubaki katika sehemu au pahala maalumu, huku akiwa ameshikamana na jambo maalumu ndani ya mahala hapo, lakini neno hili kitaalamu (kwenye fani ya sheria za Kiislam) linamaanisha kule mtu kukaa katika sehemu takatifu kwa ajili ya ...
  • je kitabu cha tarehe kijulikanacho kwa jina la Taarekhu-Tabari, ni kitabu kinachoaminika?
    10553 امام حسین قبل از امامت 2012/05/23
    Pale kitabu fulani kinaposemekana kuwa ni chenye kuaminika, huwa haimaanishi kuwa kila kilichomo ndani yake ni sahihi. Kitabu Taarikhut-Tabariy, si chenye kuepukana na usemi huu, bali nacho pia hakikubeba ndani yake yale yalio sahihi tu. La pili ni kwamba: kauli hiyo ulioinukuu kutoka katika kitabu hicho ...
  • je ni kweli kuwa Maimamu ni wabora zaidi kuliko hata Mitume?
    16934 دانش، مقام و توانایی های معصومان 2012/05/23
    Suala la Maimamu (a.s) kuwazidi Mitume katika daraja za kielimu, ni suala moja linalo onekana kuzungumziwa sana na Riwaya mbali mbali, na sababu hasa za wao kuwazidi Mitume kielimu, zinatokana na ule uhakika wa nuru ya maumbile yao, kwani uhakika wa nuru yao unatokana na uhakika wa ...
  • nini hukumu ya kufuga njiwa ndani ya sheria za Kiislamu? Na nini msingi hasa wa hukumu hiyo?
    26426 نگهداری و شکار حیوانات 2012/06/17
    Tukilitazama suala la kufunga njiwa kibinafsi, tutalikutia kuwa suala hili halina matatizo na ni halali. Lakini pale sisi tutapolimbatanisha suala hili na haki za majirani au wanajamii, hapo tunaweza kulipa picha ya uhalali au uharamu kwa jinsi hali za jamii mbali mbali zinavyolitazama suala hilo. Baadhi ya ...
  • Je ni kweli kuwa Imamu Husein (a.s) aliwahi kuwa na binti mwenye umri wa miaka mitatu au mine, aliyejulikana kwa jina la Ruqayya au Sukaina anaye semekana kuwa alifariki dunia huko Damascus?
    11645 اهل بیت و یاران 2012/05/23
    Ingawaje wengi miongoni mwa waandishi wa Historia hawakukinukuu kisa cha kuwepo kwa mtoto huyo wa kike wa Imamu Husein (a.s) mwenye umri wa kiasi cha miaka mitatu au mine, aliyejulikana kwa jina la Ruqayya au Fatimatu Sughra na baadhi ya wakati akijulikana kwa majina yasiokuwa hayo, lakini ...
  • je dini na siasa ni vyenye kuendana au vyapingana?
    14099 Elimu mpya ya Akida 2012/05/23
    Dini ni chombo maalumu kilichokuja kumkomboa mwanaadamu na kumuongoza katika njia ya mafanikio, hivyo basi ni jambo lisiloingia akilini kuwa chombo hichi kiwe ni chenye kulipa mgongo jambo muhimu linalohitajika ndani ya jamii mbali mbali, kama vile suala la usimamishaji wa serikali. Na kwa upande mwengine ni ...

YALIYOSOMWA ZAIDI